Wednesday, November 21, 2012

Shukrani kwa wale wote munayo saidia kazi zangu, Mungu awabaliki

Nataka nitowe Shukrani kwa wale wote wanao nisaidia katika kazi zangu. Nashukuru mkurugenzi wa SYUB SHOW ambao inawaburudisha habari za warundi hapa marekani na Nchi mbalimbali. katika video hiyo matangazo yangu utayaona kuanzia kwenye 5:55 

Nawashukuru na wale woooote munao tangaza kazi zangu, mukiamini yakwamba kazi zangu zina faida katika Jamii. Najua ni mupo wengi munao niombea ili niendelee mbele, nisisahau kuwa shukuru wa dau wangu wa karibu ambao munapigia simu mala kwa mala ili mujue kazi zangu zinaendeleaje, Hasasa na wale ambao mumetoa mchango ikiwa pesa ao mchango wote ule wa kuinua kazi zangu. Nawapenda sana nyote, nina imani yakwamba mutaendelea kua mashabiki, wadau hata na marafiki wa karibu sana. Maombi muhimu katika kazi kama hizi, pasipo mkono wa Mungu hatutoweza kufika pale pote. Ila kwa mkono wake, tutaweza. 

Natarajia kufanya Kolabu CD na waimbaji warundi wa nyimbo za Injili kutoka USA, kolabo hiyo ni tofauti na kolabo zingine, ila mutaona tu. Mambo ya kikamilika mutajua. musisahau kuitembelea www.burundiangospel.com maana ni moja wapo wa kazi zangu, sasa wadau mukiitembelea muna niinua kama kawaida. 

Amani ya BWANA awe nanyi 
The Superlative Kaburungu