Friday, October 5, 2012

Ikingera, wimbo katika Album natarajia kuwapa karibuni ivi

Romans 7:14-25, Hebrews 12:1

Ndugu wadau, nawasalimu wote kwa Jina La Yesu! Huu ni wimbo nilio aidi wadau wangu kua nitawatilia kwenye Youtube kabla ya kuondoa album. Nime aidi nyimbo mbili tu, ila kwanza nawatilia huu, mwingine nitatia badaye. wimbo huu nimeurikodi katika studio ya Methusela Nzisabira (GAP Studio "Glory Ambassadors Pro Studio") mjini Dallas, Tx. Baada ya mkutano mwezi wa 7 mwaka huu wa 2012 nikaona nitembelee studio ya Kijana huu kama mrundi mwenzetu na tangu apo tukawa marafiki na kuanza kuongea mengi kuhusu utengenezaji wa Audio. Vyombo katika wimbo huu vilipigwa na mimi pamoja na Methusela nzisabira, masauti yote ni mimi mwenyewe Kaburungu. sirikilizeni na mujifunze. 

Utumwa katika wimbo huu nikwamba mala tunakutana na majaribu mengi na mambo yanao tuzuwia kuifanya kazi ya Mungu, kama facebook, simu, Internet. Wakristo unakuta tunatumia mda wote wetu kwa mambo hayo badala ya kusoma biblia na kuomba, kufunga (maombi) na kumuheshimu Mungu. Kile tunacho taka kufanya sicho tunacho fanya. Tamaa za mwili zimetuteka. Wengi tulibadilisha maumbile yetu, wengine tunavaa nguo zisizo pendeza (aibu mwanamke kuvaa suruwali, nguo kama mini, hereni na mengeneo hivi ya kufanana), wengi tunadai yakwamba Mungu anaangalia moyo pekee ila anaangalia vyote ( Ezekiel 44:9) kuingia katika ufalme wa mbigu ni razima uwe safi mwilini na moyoni. Si hayo tu, kuna ukahaba, uzinzi, uongo, umbea, ujambazi, mambo ya kisani, na mengi ya kufanana na dhambi. Ni bora tujiepushe nayo maana tumesha tekwa na minyororo ya shetani kama vile anatuendesha kama gali mbovu. ni vizuri tujiangalie mambo tunayo yatenda tusije tukajikuta ni watumwa wa shetani. Wewe kuimba, kuhubiri, kufanya kazi furani ya Mungu haikufanyi kua uko msafi, kama bado una tendo la kufanana na ndambi bado wewe ni mtumwa wa shetani. Tumefungwa na tamaa za mwili ndio maana hatuwezi kuona ni wapi tunaelekea pasipo kufungua macho ya kiroho tujue ni wapi tumekosea na tumurudilie Bwana. Mafanikio na mazuri yatakua mbele zetu ila matendo yetu mabaya ndo yanatusababishia mikosi, magonjwa, laana, shida mbalimbali (Jeremiah 4:18); ndo malipo ya ubaya wetu. utavuna ulicho panda ndugu yangu. Tutambue na Shetani (kutumia Antikisto) anafanya miujiza, si kila jibu lote limetoka kwa Mungu, tafadhari jaribu kwanza ukajue jibu limetoka wapi. Unapo omba shetani huwa anasikia maombi yako, badala ya Mungu kukujibu shetani atajipendekeza ili aweze kupata njia ya kukuharibu. Ndo badaye sasa utaanza kulalamika eti kwanini Mungu amenijibu na ikaharibika ao ikageuka kua kikwazo? Mungu akijibu anajibu wala hakuna mabadiliko, tukimtii na kuziendea njia zake zote za haki, mkono wake utakua nasi milele daima. Ni vyema sasa ujichunguze vizuri mala kwa mala ili uhakikishe kabisa unatembea katika mapenzi ya Mungu. 

Burudikeni na wimbo huu, pia muniombee ili Album nije niitoe salama. Kama unataka kusaidia, msaada pia unaitajika. Ikiwa ni kwa maombi ao kwa kila kitu chochote kile, kikitokea moyoni mwako, Tuatabalikiwa wote. Tusisikilize tu bila kujifunza, bali tusikie na tujifunze, maana Yesu alisema heri anaye sikia na kutenda (Kusikiriza na kutenda). Tuambiane pia tushauriane wote, kama umefanikiwa kusikia wimbo huu, basi utangazie kwa majirani na ndungu na Jamaa utabalikiwa, maana utakua unaitangaza Injiri ya Bwana kama vile alivyo sema; "Enendeni Muyageuze mataifa yote kua wanafunzi wangu! mujuwe hili: nipo pamoja nanyi siku zote, hadi siku za mwisho" Yesu kasema! 

Mbalikiwe 
The Superlative Kaburungu  

Wimbo ulio changanya wadau wengi

Ndugu wadau na mashabiki, marafiki na jamaa, hii ni wimbo nilio imba mwaka wa 2010 nikiwa katika mjini Seattle, WA baada ya kuondowa Album yangu ya kwanza "Uruwo Gushimwa" mwaka wa 2009. Basi nikataka kuifanya Album ingine ya pili nikaandaa wimbo huu ila Mungu akaniita nifanye kazi furani ya uhubiri na mambo mengineo. Rakini hata ivyo nimepewa neema kutoka kwa bwana niko natengeneza Album mpya "Music Video" karibuni mwaka wa 2013, kwa sababu naisubiria Album nilio tengeneza na Kwaya Hossana apo Seattle, WA iondolewe. 

Wadau wengi hua wanasema hii nyimbo ni ya mapenzi, labda kwasababu mwendo wa nyimbo unafanana na Hip Hop ao kama nyimbo za kisani. Kipaji nilicho nacho naweza kuimba katika Style yote ile ingawa si style zote ila nimefanikiwa kuimba katika style nyingi. Hii wimbo si ya mapenzi ila ni ya kushauri Jamii: "urukundo nagukunze ngo tubane amahoro, ariko ukampora uwo ndiwe, ubwoko nakaranga." Katika jamii zetu za kisasa watu huzarauwana ao kuchukiana kutokana na ukabira wa mtu ila sisi wote tumeumbwa na Mungu mja. uwe muisilamu, uwe mukristo, uwe na dini gani ao kabira ipi, ujuwe yakwamba sote tumeumbwa na Mungu mmoja alie hai, Muumba wa mbingu na Inchi maana Dunia na vilivyomo ni mali ya bwana. Tupendane, tusichukiane, kama Nchi zetu za Africa, tuwe na umoja katika maendeleo ya kimaisha. tusibaguwane wala tutengene, tujue upendo wa Mungu jinsi alivyo tupenda bila upendeleo, anamwinua anaye mtaka na anamushusha anaye mtaka. Mawazo yake na njia zake sikama za mwanadamu. Basi tufuate mtindo huo wa Yesu. 

Naimani tumeelewa ya kwamba wimbo huu si wa mapenzi ao nini, ila ni ushauri kwa Jamii zetu. Walio kua na maswali na Imani mmelizika na nawashukuru kwa support yenu na maombi yenu ili kazi ya Mungu iendelee, tuendelee kupendana hadi mwisho wadunia. 

Mungu awape balaka na Hekima
The Superlative Kaburungu