Monday, October 1, 2012

Wa dada zetu warundi walituaga duniani

Wa dada wenzetu "Vestina & Violette" walikua wana ishi mjini Amarillo, Texas. Wasichana hawa walikua na umri mdogo kama 11 ao 12-13, waliiaga dunia tarehe 30 mwezi wa 9 mwaka huu wa 2012 masaha ya jioni kuanzi kama sa 8pm.  

Habari zina twambia yakwamba waliuwawa baada ya hajari, tena alie wagonga hakusimama aliendelea kuitembeza gali bila kuwajari. Baada ya kugongwa wasichana hao walisimama na kumbea ili watoke balabalani, cha kushangaza na kuuma nikwamba walipo vuka balabalani wakauwawa. Mmoja aliuwawa aipo fika kwenye ukuta ao uzio (Fence, kirundi: urupango) kwa wajirani, mwengine akaja kuuwawa polini (nahisi alikua njiani akielekea nyumbani) 

Kinacho nisikitisha, hawa madogo zetu (wasichana) katika kutembea kwao walikua wanatokea kusukwa meshi na mama mmoja hivi kama jirani yao. Sasa ndipo walipokua wanaelekea nyumbani wakapatwa na hajari hiyo. 

Nataka nitoe mashauri kidogo wa dada zetu tulio fanikiwa kupata pumzi leo na tumushukuru Mungu kwa hilo. Dada zetu, naomba tuisikie sauti yabwana tunapo shauriwa, nikwamba tulifika huku malekani, tukaanza kubadilisha mwili yetu, wengine kugeuza nywere na mengi zaidi furani. Jamani Bwana alisema kua tukifika katika nchi hizi na kujigeuza kiukweli tutashuhudia mkono wake na tutahukumiwa. usingojee eti kutakuwa na mwisho wa dunia ndo tunyakuliwe; Bwana wetu Yesu alisema, palipo wawili patanyakuliwa mmoja, na palipo watatu ao ine, tano, sita kuendelea, patanyakuliwa wachache wengine wabaki. Ukiona nalia kanisani usinishangae, nawalilia ndungu zangu, walio fungwa na dawa za kurevya, washerati, waongo, wazinzi, makahaba, majambazi, wauwaji, na mengineo yakufanana na dhambi, ili waokoke. Nawalilia pia ndungu zetu walio fika uku malekani wakaa kubadilisha myili yao kua byashara, wengine wakasuka meshi, wanawake kuvaa ma suluwali na hereni na mengineo zaidi ya kuchafua mwili yao. Je hatujui yakwamba mwili yetu ni hekaru la loho mtakatifu? Hata na wanaume wengine wamefuatia mtendo huo wakuvaa hereni na wengine kuvaa nguo zao kinyume na heshima kama mkristo ao kama mwanadamu alie umbwa na Mungu. Tafakarini siku tunazo nichache sana, Hujui ni lini siku yako. tumewakosa dada zetu "Vestine and Violette" Je ninani anajua Mwisho wao? Mungu pekee. Kinacho nisikitisha waliuwawa na meshi kichwani, na alie wasuka meshi hizo hua na yeye damu zao zitamfuata. Heri amrudilie Bwana mapema atubu dhambi zake, na si vyema kuasuka meshi wengine maana unaunga mkono mwovu shetani pia unasababisha wengine kuyaona mapigo ya Bwana. Bora kuwashauri  na kuwafundisha njia za Bwana badala ya kuwasuka. Jiulize mwenzangu, ukifa leo, utakuwa mgeni wanani? mambo unayo yatenda mwenyewe unajua, Je utapokelewa na wanani? Mashetani ao malaika za Bwana? Jiangalie katika nyenendo na matendo maana mwisho tumesha ufikia usingojee eti unakaribia, na sisi tunaelekea huko, Swali kwako; Je utakua mgeni wa nani? Sisi tulio ukoka tutakua wageni wa Yesu, mkubali yesu kua Bwana na Mwokozi wa maisha yako akusemehe dhambi ulizozitenda. Kifo hakijari umri wala masomo wala uzuri wako, kifo wala hakitajwi eti sijaowa sina watoto, kifo hakina huruma. Shetani anazunguka kuzitafuta roho zawatu nawaoneya huruma mnao mkataa yesu. 


Vifo vya kujitukiza duniani Vime enea, Jana alikua mzima leo tunaambiwa kafa. Ukimwona kwenye jeneza, utazani ataamka , mtu na hafya yake kaburini anakwenda. Ndugu zangu ni heri tutengane na Dhambi tumrudilie bwana mapema, yuwaja mawinguni, leo ni hawa dada zetu kesho ni sisi, Je tutapokelewa na nani? 


Mungu uzilaze mahali pema peponi roho za wadada zetu "Vestine & Violette". Nawaombea balaka na faraja kutoka kwako Yesu, wazazi na ndugu na marafiki wawalio achwa na dada zetu. Acha uwitwe Mungu maana ndivyo ulivyo. Uokowe nafsi zetu pia uponye roho na mwili vyetu, sifa na utukufu vikurudie Bwana ambae unatoa na unatwaa. Nani wakukupinga? Njia zako sikama za mwanadamu, na mawazo yako si kama ya mwanadamu. Mungu uwimidiwe daima Amen. 

The Superlative Kaburungu