Friday, December 31, 2010

Mwaka mupya na mambo mapya.

Ndugu wapendwa pamoja na wadau wangu wote, nashukuru kwa musaada wenu kwa kunipa matumaini kua nitaendelea vizuri. Pia na toa shukurani kubwa sana kwa Mungu alie sababisha haya yote nakunipa uwezo wa kutenda haya yote, na namuomba mwaka huu wa 2011 uwe mwaka wa mambo mapya na balaka zaidi. 


Tunashukuru Mungu anaye tupitisha katika mwaka unayo pita, kweli kabisa tulifanya mengi japo shetani aliharibu ila Mungu anatupigania siku kwa siku. jamani mwaka mupya na mambo mapya. sasa tugeuke tuwache ujinga wa mwaka ulio pita tuka anze na mwaka wa 2011. nahisi kua huu mwaka utakua mwa muziri sana kwa kua na anza maisha upya tena na badaliko pia na balaka za Mungu. Nashukuru Mungu kwa hilo.


Katika kuigiza kwangu, naomba Mungu awe mwanzo kwa kila jambo nitakalo lifanya. filamu zangu zikawafundishe yalio mema na kuepukana na mabaya. Na aidi wadau wangu na mashabiki na ndugu wapendwa kua movies zangu zinaenda kua bora zaidi na quality ya hali ya juu. na kwa kuaonyesha ivo nimewawekea community (UGLEA World Community - ugleaworld.ning.com) kuwaonyesha kua tunaenda kushirikiana na wa artists wote kwa pamoja tukawape burudani. movies zangu nyingi tena bora zaidi zina karibia. nitafurahi sana wadau mukinisaidia kwa kununua na ku support.


katika kuimba kwangu, nafurahi tena kwa vile na muimbia Mungu. naimba Gospel Songs and Worship songs. mala kwa mala utakuta na rap ila maneno ni mungu. wadau nyimbo zangu za mwaka huu ziwafundishe na mupate balaka Mungu akawasaidie sana katika mambo yote munayo fanya.


huu ni mwaka mupya na mambo mapya. kama unahisi kuna kitu unataka kufanya ila huna uwezo. usi site kuniita tukasaidiane. nipo kwalo njo pamoja tumwombe Mungu atupe balaka na mafanikio. huu ni mwaka mupya na ningependa wote tumukalibishe Yesu kua mwokozi wetu wa maisha yetu. kama una shida una kitu unataka kufanya ila shetani amekutenga nacho, na unaitaji musaada wa maombi, karibu nipo muda wowote, njoo tukamwombe Mungu naye atatenda! 


Asanteni nyote nawatakia mema katika mwaka huu wa 2011


-The Superlative Kaburungu-